2 Desemba 2025 - 23:48
"Kielelezo cha Ushujaa na Subira ya Mama za Mashahidi/Riwaya ya Mama wa Mashahidi Wawili wa Lebanon, Kuanzia Malezi ya Kiashura hadi Subira ya Zaynab"

Mama wa mashahidi wawili wa Lebanon, katika mahojiano na ABNA, alisimulia uzoefu wake kama mama katika njia ya muqawama na uvumilivu aliokuwa nao baada ya kuwapoteza watoto wake. Pia aliwasihi mama na wake za mashahidi waendelee kufuata njia ya wapendwa wao na kushikamana na imani.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) -ABNA-: Katika kumbukumbu ya siku ya kufariki kwa Bibi Ummul-Banin (a.s)، mwanamke ambaye jina lake limeunganishwa na uaminifu, kujitolea, na uzazi wa mashujaa, na katika siku ambayo inaheshimiwa kama siku ya kuwakumbuka na kuwatunuku heshima mama na wake za mashahidi, tulimtembelea mmoja wa nyota angavu wa njia hii؛ Bibi Aida Sarour, mwanamke kutoka kusini mwa Lebanon ambaye maisha yake ni kioo hai cha maana ya “umama katika medani ya muqawama”.

Aida Sarour, aliyezaliwa mwaka 1971, aliingia ujana katika kipindi ambacho Lebanon ilikuwa ikivuta pumzi chini ya kivuli cha vita na uvamizi؛ lakini upepo wa Mapinduzi ya Kiislamu kutoka Iran hadi Beirut ulikuwa umefika, ukiwapa vijana wa eneo hilo roho mpya. Katika mtazamo wa Imam Khomeini (r.a)، aliona nuru na mvuto uleule aliokuwa ameupata katika macho ya Imam Musa Sadr؛ nuru iliyoangaza njia yake kuelekea kwenye muqawama. Aida alitoka katika familia rahisi، lakini alifanya uchaguzi mkubwa؛ uchaguzi wa kuishi ndani ya mzunguko wa imani na kusimama kidete.

Aliolewa na mmoja wa mujahidina wa Hizbullah na akawa mama wa watoto ambao kila mmoja alikua katika njia hiyo ya mapambano. Mtoto wake mdogo, Ali Abbas Ismail, alifikia shahada akiwa na umri wa miaka kumi na nane, katika ulinzi wa haram. Uhusiano wa karibu na wenye kutia nguvu wa Aida na Ali unaonyesha sura ya kina ya utu wa Aida؛ mama mwenye upendo, ufahamu na uthabiti, aliyewalea watoto wake si kwa ajili ya vita، bali kwa ajili ya uhuru, heshima na uaminifu kwa haki. Katika njia hii, sasa yeye ni mama wa Mashahidi wawili na ana nafasi muhimu katika shughuli za kitamaduni na kijamii za muqawama nchini Lebanon.

Leo، Aida Sarour si tu “mama wa shahidi”؛ yeye ni kielelezo cha kizazi cha wanawake wa Lebanon na wanawake wa maeneo yote ya muqawama، ambao kwa subira na ujasiri wao wamekuwa nguzo imara za njia hii. Wanawake ambao, licha ya maisha ya kawaida yaliyojaa upendo، wameandika vitendo vikubwa zaidi vya kujitolea katika zama zetu. Uwepo wake katika mahojiano haya ni kutolea heshima hadhi ya wanawake ambao kama Bi Fatima (a.s)، Bi Zaynab (a.s) na Bibi Ummul-Banin (a.s)، ni wabebaji wa ujumbe wa uaminifu, ujasiri na umama wa Kiashura.

Tajiriba ya mama wa mashahidi wawili؛ uchaguzi wa kimungu na imani ya umama

Aida Sarour kuhusu uzoefu wake wa kuwa mama wa mashahidi wawili alisema:
“Ni neema kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwamba Akanichagua miongoni mwa familia za mashahidi، na kwa kufikia shahada kwa wana wangu wawili، Muhammad Ali na Ali، Akanipa heshima hiyo. Mimi kama mama، kama mama wengine wote، nina hisia—hisia za kimama na za kina. Lakini pale dini inaposhinda hisia hizi، najisema: ‘Ewe umama، toa njia, kwa kuwa sasa ni mwito wa dini ya Muhammad na Aali Muhammad: Ewe Mola، mtumie rehema Muhammad na Aali Muhammad.’”

Akaendelea:
“Mimi ni mtu niliyewakabidhi watoto wangu kwa hiari yangu mwenyewe، bila kungoja amri ya mtu yeyote، katika sadaka ya mapenzi ya Mungu. Kinyume chake، ni mimi mwenyewe niliyefanya uamuzi huo؛ kwa sababu mimi ni mama niliyeamini kwa dhati katika Mungu، Siku ya Kiyama na Siku ya Ahadi. Siku hii ya ahadi، ambayo sote tutaifikia، ndiyo siku ambayo tumewatoa watoto wetu kwa ajili yake. Imani hii imekita mizizi katika mioyo yetu na katika mtindo wa maisha yetu tangu utotoni، na imeunda njia ya maisha yangu.”

Wakati wa kupokea habari za shahada

Aida Sarour alisimulia wakati alipousikia habari za kufariki kwa mwanawe:
“Nilikuwapo katika haram ya Imam Ridha (a.s)، katika Baab al-Jawad، wakati habari za shahada ya mwanangu zilipofika. Nilisikia sauti ikilitaja jina la Muhammad Ali، sauti ileile ya jina la mwanangu. Kuba ya haram ilikuwa iking’aa mbele yangu، nikasema moyoni: ‘Ee Mola، siku zote nimekuambia: Chukua mpaka uridhike.’ Na sasa ninayaweka mambo yangu yote mikononi mwa Mwenyezi Mungu، Msimamiaji wa mambo yote.”

Akaongeza:
“Niliionea haya kupiga ukemi au kulia، kwa kuwa nilikuwa mbele ya Imam Maasum na mlangoni kwa mwanawe، Imam Jawad (a.s)، nami nikayaacha yote kwenye makadirio ya Mwenyezi Mungu.”

Mapenzi ya Mungu؛ sifa kuu ya watoto wake

Alieleza sifa mashuhuri zaidi za watoto wake kwa kusema:
“Sifa yao kubwa ilikuwa mapenzi kwa Mungu. Mungu aliwapenda، nao pia walimpenda Mungu؛ ndiyo maana kutoka kwa watoto wangu na familia yangu، Mungu alichagua mashahidi. Mimi nimewaachia watoto wangu urithi wa kumpenda Mungu؛ nimewakunywesha maziwa ya mapenzi ya Mungu na mahaba ya Muhammad na Aali Muhammad. Kwa hiyo ni jambo la kawaida kuwa njia yao ingeishia kwenye shahada.”

"Kielelezo cha Ushujaa na Subira ya Mama za Mashahidi/Riwaya ya Mama wa Mashahidi Wawili wa Lebanon, Kuanzia Malezi ya Kiashura hadi Subira ya Zaynab"

Subira na Ustahimilivu؛ Mafundisho ya Kiashura

Kuhusu iwapo alihisi maumivu au huzuni baada ya kumtoa mwanawe kwa ajili ya Mwenyezi Mungu, alisema:
“Kamwe؛ mimi niliwakabidhi watoto wangu kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kila kilichotolewa kwa ajili ya Mungu hukua. Kwa mapenzi ya Mungu, Yeye ndiye anayetoa subira. Kigezo changu ni Bibi Fatima Zahra (a.s)؛ ninawezaje kusema nina huzuni au nimechoka؟ Naona haya kusema kuwa mimi ni mfuasi wa Fatima au Zaynab, halafu niseme: ‘Mola wangu, ninahisi uchovu.’ Njia hii ni njia ya imani na ustahimilivu, na kwa fadhila ya Mungu itaendelea.”

Aida Sarour aliendelea:
“Kwa msingi wa uzoefu wangu، nawaambia akina mama kwamba hili ndilo jambo ambalo Kiongozi wetu، Imam Khomeini (q.s)، alilisema: Kila tulichonacho kimetokana na Ashura؛ na kila mnachonacho ninyi kimetokana na Ashura. Ashura ni mwendelezo ulio hai katika zama zetu. Tunapohudhuria majlisi za Aba Abdillah al-Husayn (a.s) na kusikia maneno yake، tunapaswa kuyafanya mafunzo hayo kuwa sehemu ya maisha yetu. Sio tu tunapoisoma Ziyarat Ashura na kusema: ‘Laiti ningalikuwa pamoja nawe,’ bali tunapaswa kusema pia kwa ukweli: ‘Laiti tungalikuwa pamoja nawe katika maneno na matendo.’ Na inshaAllah، pale mama anapokuwa miongoni mwa Zaynabiyyat، ataweza kuwa kama Bibi Zaynab (a.s)، na msimamo wake katika mashaka utakuwa sawa na msimamo wake katika siku ya kumi ya Ashura: ‘Mola wangu، chukua mpaka uridhike.’”

Ushauri kwa Mama za Mashahidi؛ Kuendeleza Njia ya Mashahidi

Aida Sarour kuhusu nasaha zake kwa mama za mashahidi alisema:
“Nawasihi akina mama wote، na hasa mama za mashahidi، watambue kwamba shahidi hutoka duniani kwa ajili ya lengo tukufu، na lengo hilo halipaswi kuzimika baada ya shahada yake. Mama anapaswa kuwa mtu wa kubeba jukumu، kuchukua msimamo، na kuendeleza njia ya mwanawe. Huenda sisi tusiwe katika safu ya mbele، lakini tunaweza kuifanya njia yao ibaki hai.”

Akaongeza:
“Vile Imam Khomeini (r.a) alivyosena: Wakati shahidi anapofikia shahada، damu yake huzaa matunda mbele ya Mwenyezi Mungu، lakini pia kalamu na neno safi huinuka kwenda kwake. Nasi kwa kutekeleza maagizo ya Ayatullah Khamenei—Mwenyezi Mungu amzidishie maisha—tunashiriki katika jihadi ya uelimishaji na ufafanuzi. Ndipo hapa inapopatikana nafasi ya mama za mashahidi؛ nafasi yao ni kuendeleza njia za watoto wao na kukamilisha safari tukufu ambayo shahidi ameianza.”

"Kielelezo cha Ushujaa na Subira ya Mama za Mashahidi/Riwaya ya Mama wa Mashahidi Wawili wa Lebanon, Kuanzia Malezi ya Kiashura hadi Subira ya Zaynab"

Watu wa Kutenda Wajibu na Kushikamana na Njia ya Mashahidi

Aida Sarour kuhusu hali ya muqawama nchini Lebanon mbele ya shinikizo la Marekani na utawala wa Kizayuni alisema:
“Huu ni msimamo wenye busara kabisa. Katibu Mkuu wetu, Sheikh Naeem Qassem, na viongozi wengine wa muqawama wana uzoefu na hekima kubwa, na wamekuwa katika jihadi kabla yetu. Ingawa adui huzunguka atakavyo na anamiliki maghala makubwa zaidi ya silaha duniani, sisi tunacho kitu chenye nguvu kuliko haya yote: imani kwa Mungu na utiifu kwa uongozi. Sisi kila mara tunatekeleza wajibu wetu, na kama Sayyid Hassan Nasrallah alivyosisitiza, popote inapolazimu tupo. Sasa si wakati wa vita ya moja kwa moja, lakini sisi daima ni watu wa kutenda wajibu na kushikamana na njia iliyo sahihi.”

Tutakuwa Kila Wakati Katika Safu ya Mbele

Kuhusu hali ya Lebanon na shinikizo la kimataifa, alisema:
“Serikali ya Lebanon imetuvunja moyo. Leo kana kwamba mataifa yote ya dunia yameungana dhidi ya Lebanon. Laiti kungekuwa na chembe ya huruma kwa watu wa Lebanon, lakini kwa masikitiko, roho za wengi hununuliwa kwa fedha, madaraka na vyeo. Alhamdulillah sisi si miongoni mwa roho hizo؛ roho ambazo haziwezi kununuliwa kwa pesa wala kwa ahadi yoyote ya dunia.”

Akaendelea:
“Mheshimiwa Katibu Mkuu katika hotuba yake ya mwisho, takribani wiki mbili zilizopita, alisema kuwa tumeufikia wakati ambao huenda subira yetu ikaisha. Kauli hii ilikuwa tishio wazi lakini lililopimwa vizuri. Adui, pamoja na wale wanaoshirikiana naye ndani ya nchi, wanapaswa kufahamu kuwa wakati na mahali pa majibu vitachaguliwa na muqawama. Tuko tayari؛ na ikifika saa yake, watu na muqawama, kama ilivyokuwa daima, watasimama kwenye safu ya mbele.”

Hadithi ya Kukutana na Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu

Aida Sarour kuhusu kukutana kwake na Kiongozi Muadhamu alisema:
“Nilienda Iran kwa ajili ya kuchapisha kitabu kuhusu mwanangu, shahidi wangu wa kwanza, Shahidi Ali. Siku chache baadaye, nilisafiri kutoka Tehran kwenda Mashhad، na wakati huohuo ndipo habari za shahada ya Shahidi Muhammad Ali ziliponifikia—jioni ya siku hiyo hiyo. Tulipaswa kukutana na Kiongozi Muadhamu kwa kuwa mimi ni mama wa shahidi, na mkutano huo uliadhimishwa katika siku za Fatimiyya. Tulikuwa wageni wao kwa muda wa siku tatu katika Husayniyya ya Imam Khomeini.”

Akaendelea kusema:
“Siku ya kwanza, nilipoingia kwenye kikao cha faragha, nilimsalimia na nikamwambia: Leo mwanangu Muhammad Ali amefikia shahada. Akachukua pete niliyokuwa nimewahi kumpa aiombee baraka، akaiombea na akasema: InshaAllah yeye ni mujahidi wa njia ya haki kuelekea Quds. Nikamwambia: Ndiyo. Pete hiyo kila mara ilikuwa mkononi mwa Muhammad Ali، lakini siku ya mwisho ya safari aliisahau nyumbani، na hapo ndipo alipofikia shahada. Tulipoenda Mashhad، tulikaa siku tatu katika Husayniyya wakati wa Fatimiyya، na niliombwa kutoa hotuba katika sherehe ya kuzaliwa kwa Bibi Fatima Zahra (a.s). Nilihisi kana kwamba nimetoka katika dunia hii ya udongo na kuingia katika ulimwengu wa malakuti. Kwa upendo wote nilitazama uso wake wa kipeponi، na nikatoa hotuba bila karatasi wala kalamu. Nilipotazama macho yake yaliyojaa mwanga wa Kipepo، nilihisi niko mbele ya mmoja wa waja wateule wa Mungu، na mbele ya naibu wa Sahib al-Zaman.”

Kushikamana na Ardhi na Ushauri kwa Watu wa Iran

Aida Sarour aliongeza:
“Mimi natoka kusini mwa Lebanon، katika kijiji kilicho karibu na mpaka wa maeneo ya Palestina yaliyokaliwa kwa mabavu. Sisi tunasema ardhi ya Palestina imetekwa، na damu ya mashahidi kila mara huzaa ushindi. Ardhi hii imelewa kwa damu ya mashahidi، na kushikamana kwetu na ardhi hii ni urithi wa mababu zetu.”

Mwisho, akiwahutubu watu wa Iran، alisema:
“Jitanzeni kuwa wafuasi wa kiroho wa Wali wa Mungu na Kiongozi wa Iran. Yeye ana nafasi ya baba mwema kwa wote، wakubwa kwa wadogo. Na kwa jukwaa zima la muqawama، kuanzia Yemen hadi Gaza na Iraq, na kwa wapiganaji wote pamoja na wazazi wao، ninatoa nasaha ya kuwa na subira na ustahimilivu، kwa kuwa Mungu yu pamoja na wenye subira. Tukivumilia -sisi na ninyi- InshaAllah ushindi utakuwa wa washirika wetu. Mwenyezi Mungu awakuzeni kwa heshima.”

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha